Magufuli atikisa Kilimanjaro
Magufuli akiwaeleza wakazi wa Ndungu Same Mashariki, uchapakazi wa Anne Kilango na jinsi atakavyoshirikiana nae kiukaribu kwa maendeleo ya jimbo la Same Mashariki endapo atakuwa rais.
Akizungumza na wakazi hao Magufuli aliendelea kunadi sera zake za kutengeneza barabara za lami maeneo hayo, kumaliza migogoro ya ardhi, kutatua tatizo sugu la maji, kupunguza kodi ya pembejeo za kilimo na dawa za mifugo.
Magufuli aliwaahidi wananchi hao kuibadilisha Tanzania na kuwa mpya yenye neema huku akifafanua jinsi atakavyoleta mabadiliko.
PICHA NA RICHARD BUKOS/GPL ALIYEKUWA KILIMANJARO