MAKAMU WA RAIS WA TANZANIA, SAMIA SULUHU AWASILI, ZANZIBAR LEO
Makamu wa rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amewasili leo jioni katika uwanja wa ndege wa Zanzibar, akiwa ameambatana na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, kwa ajili ya kuhudhuria hafla mbili za kitaifa, kuhitimisha kilele cha Mwenge na kuadhimisha kumbukumbu ya kifo cha baba wa Taifa, Mwl Julius Nyerere, zikazofanyika kesho katika uwanja wa Aman uliopo katika mkoa wa Mjini Magharibi.
Mama Samia na RC Makonda wamepokelewa na mwenyeji wao, mkuu wa mkoa wa Mjini Magharibi, Ayoub Mohammed Mahmoud, ambaye aliwashukuru kwa kuwasili kwao Zanzibar na kuahidi kushirikiana nao kikamilifu katika shughuli ya kesho.
NA ISRI MOHAMED/GPL