The House of Favourite Newspapers

Makonda Apokea Misaada ya Waathirika wa Mafuriko Dar

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, akizungumza jambo na viongozi wa taasisi mbili za Abdullah Aid Emergency Appeal na ya Darul Irshad Islamic Centre kabla ya kupokea misaada ya magodoro na vyakula kwa ajili ya waathirika wa mafuriko yaliyotokana na mvua kubwa jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya magari yaliyobeba misaada hiyo.
 Makonda akipokea msaada kutoka kwa Arif Yusuf ( wa tatu kushoto) wa Taasisi ya Dural Irshad Islamic Centre.
…Akipokea msaada kutoka mwakilishi wa Taasisi ya Abdullah Aid Emergency Appeal.
Mwenyekiti wa  Taasisi ya Dural Irshad Islamic Centre, Arif  Yusuf ,  akizungumza jambo.
Makonda akiendelea kupokea misaada.
…Akipokea misaada ya vyakula.
Makonda (katikati) akiwa katika picha  na baadhi ya wawakilishi wa taasisi hizo mbili waliotoa misaada hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, leo Aprili 26, 2018, amepokea msaada wa magodoro, neti na vyakula kutoka kwa taasisi mbili tofauti zilizotokea Zanzibar; moja ni Abdullah Aid Emergency Appeal na Darul Irshad Islamic Centre kwa ajili ya kuwasaidia waathirika wa mafuriko waliopoteza mali zao hivi karibuni kutokana na mvua zilizonyesha mfululizo kwa zaidi ya siku tatu.

 

Baada ya kupokea msaada huo, Makonda amezishukuru taasisi hizo na kuweka wazi kuwa misaada hiyo itakwenda kwa waathirika wa mafuriko ambao nyumba zao hazipo mabondeni, kwani wale ambao wanaishi mabondeni wamekiuka agizo la serikali la kuwataka wahame kabla ya mafuriko kuwakuta.

Comments are closed.