The House of Favourite Newspapers

Malaika afurahia kuwa singo

0

MALAIKAMSANII anayefanya vizuri katika Bongo Fleva, Malaika Exavery amedai anafurahia maisha ya kutokuwa na mpenzi, kwani anakuwa huru kufanya mambo yake bila kuingiliwa na mtu.

Akizungumza na Risasi Vibes, Malaika alisema baada ya kutemana na mpenzi wake wa siku nyingi, Eddy anaona tofauti kubwa kwani kuna vitu ambavyo nafsi yake inapenda kuvifanya na anavifavya.

“Kwa kweli nitachukua muda sana kuanzisha uhusiano mwingine mpya, nafurahia mno maisha yangu ya sasa, niko huru kufanya vitu vyangu navyovipenda toka ndani ya moyo wangu,” alisema msanii huyo anayetamba na kibao chake cha Rarua.

Leave A Reply