Manchester United watinga fainali FA
Louis van Gaal na Martial wakifurahi baada ya ushindi kwenye kombe la FA uwanja wa Wembley
Anthony Martial akishangilia gori lake liliipeleka manchester united finali
Timothy Fosu -Mensah, Daley Blind, Antonio Valencia, Marcos Rojo, Chris Smalling and Martial wakishangilia baada ya kuingia fainali kombe la FA
David de Gea akiruka upande wa kulia kuiokoa penati iliyopigwa na Romelu Lukaku
Marouane Fellain akishangilia gori la kwanza katika mchezo wa nusu fainali kati ya Everton na Manchester United
David de Gea akishangilia gori lililofungwa na Anthony Martial dakika za majeruhi
wachezaji wa Everton wakiuzunika baada ya kuondolea kwenye kombe la FA
Bao la lala salama la Antony Martial limeipa rekodi Manchester United kucheza fainali ya 19 ya FA Cup kufuatia ushindi wa Everton kwenye uwanja wa Wembley.
Martial alikihakikishia ushindi kikosi cha Louis van Gaal ambacho sasa kitakutana na Crystal Palace au Watford kwenye mchezo wa fainali.
Marouane Fellaini aliifungia United bao la kuiongoza kwa shuti la karibu lakini shukrani za United zinakwenda kwa David de Gea aliyeokoa penati ya Romelu Lukaku dakika ya 57.
Everton walipata bao lao la kusawazisha zikiwa zimesalia dakika 15 mchezo kumalizika ambapo Chris Smalling alijifunga wakati akijaribu kuokoa mpira wa krosi ya Gerard Deulofeu.
Wakati mchezo ukionekana utakwenda kwenye dakika za nyongeza, Ander Herrera alipiga pasi iliyomkuta Martial ambaye aliupachika mpira kambani huku golikipa wa Evertton Joel Robles asijue cha kufanya.