Mandonga Apigwa Kwa TKO Dhidi Ya Bondia Moses Golola Kutoka Uganda – Picha
WIKI moja tu baada ya kulambishwa sakafu Nchini Kenya, bondia maarufu wa Tanzania Karim ‘Mtu Kazi’ Mandonga, amepokea kipigo kingine kwa TKO katika raundi ya pili dhidi ya Bondia Moses Golola kutoka Uganda.
Baada ya pambano Mandonga alifarijiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Amos Makalla ambaye alimwambia ‘hata hivyo Mandonga mtu kazi wewe ukipigwa ni kama umepiga na kama ukipiga ni kama umepigwa.”