The House of Favourite Newspapers

Mapambano ya Ubingwa wa Afrika Mashariki na kati Yafanyika Jijini Dar

Tonny Rashid (kushoto) akitifuana na Haidari Mchanjo.

Mapambano ya Ubingwa wa Afrika Mashariki na kati, yamefanyika kwa kishindo usiku wa kuamkia leo Agosti 24, 2019 Club 361 Mwenge jijini Dar es Salaam . Mgeni rasmi Mkuu wa Mafunzo na Utendaji Kivita Jeshini, Meja Jenerali Alfred Kapinga

Mabondia wametifuana kuwania ubingwa wa Afrika Mshariki huku wajeda nao wakijiwinda na michuano ngumi za ridhaa ya kimataifa ya majeshi yanayotarajiwa kufanyika mapema hivi karibuni.

Katika mtifuani huo mkanda wa Ubingwa Afrika Mashariki uzito wa Unyoya ulianza kupiganiwa na Issa Nampepechena Nassibu Ramadhani pambano lililokuwa na raundi kumi ambapo Nassibu aliibuka na ushindi.

 

Pambano lingine la Ubingwa wa Afrika Mashariki uzito wa Bantam nalo lilikuwa la raundi kumi kati ya bondia, Tonny Rashid na Haidari Mchanjo ambapo Tonny ndiye aliyeutwaa mkanda huo.

Mchanjo kushoto akimtupia konde Tonny.
Wakiviziana.
Tonny akivishwa mkanda wa ubingwa.
Tonny akimwaga tambo sasa.
Rais wa Shirikisho la ngumi la T.P.B.O Yasin Andallah Ostaadh akimpongeza mwamuzi mwanamke Pendo Njau kwa uwezo mkubwa aliouonesha kuliendesha pambano hilo.
Issa Nampepeche (kushoto) na Nassib Ramadhani nao walichuana vikali kugombea ubingwa wa Afrikana Mashariki uzito wa Bantam.
Wakitifuana.
Nampepeche na Nassib (kulia) wakitoa burudani.

HABARI/PICHA: RICHARD BUKOS /GPL     

Comments are closed.