The House of Favourite Newspapers

Marekani kusitisha usambazaji wa baadhi ya silaha kwa Israel iwapo itaendelea na uvamizi Rafah

0
US President Joe Biden speaks during a press conference in Seoul, South Korea, on May 21. (Saul Loeb/AFP/Getty Images)
(Photo by SAUL LOEB / AFP) (Photo by SAUL LOEB/AFP via Getty Images)

Rais Biden anaonya kuwa ataacha kusambaza baadhi ya silaha iwapo Israel itaanzisha operesheni ya ardhini.

Rais Joe Biden ameionya Israel kwamba Marekani itaacha kusambaza baadhi ya silaha iwapo itaanzisha operesheni kubwa ya ardhini katika mji wa Rafah wa Gaza.

“Ikiwa wataingia Rafah, sitoi silaha ambazo zimetumika kihistoria kukabiliana na Rafah,” alisema wakati wa mahojiano na CNN.

Aliongeza kuwa “ataendelea kuhakikisha Israel iko salama”.

Licha ya upinzani mkali wa Marekani, Israel inaonekana iko tayari kufanya uvamizi mkubwa huko Rafah.

Sehemu iliyosongamana ya kusini mwa Gaza ndiyo ngome kuu ya mwisho ya Hamas katika eneo hilo. Maafisa wa Marekani wameonya kwamba operesheni katika mji huo – ambapo idadi ya watu imeongezeka na wakimbizi kutoka maeneo mengine ya Gaza – inaweza kusababisha hasara kubwa ya raia.

“Hatutasambaza silaha na makombora ya mizinga,” Bw Biden alisema katika mahojiano hayo yaliyopeperushwa Jumatano.

Alisema Marekani haikufafanua hali ya sasa ya Rafah kama operesheni ya chinichini. “Hawajaingia katika maeneo yenye watu. Walichokifanya ni kufika mpakani,” alisema.

“Lakini nimeweka wazi kwa [Waziri Mkuu wa Israel Netanyahu] na baraza la mawaziri la vita, hawatapata uungwaji mkono wetu, kama kweli wataenda katika maeneo yenye watu.”

Bw Biden alikiri kwamba silaha za Marekani zilitumiwa na Israel kuwaua raia huko Gaza.

Alipoulizwa kama Israel imevuka “mpaka”, rais wa Marekani alijibu “bado”.

H BABA AJILIPUA MAZITO-HARMONIZE-DIAMOND-PAULA NA MARIOO KUHUSU NDOA | HOTPOT

Leave A Reply