Mastaa Wamiminika Uzinduzi wa Juice Kingdom Tabata, Usipime!
JANA, Tabata- Segerea jijini hapa kulikuwa na uzinduzi baab’kubwa wa kinywaji freshi ambapo Juice Kingdom, chini ya Mkurugenzi wake Zabron Julius walikuwa wanazindua tawi jipya.
Katika uzinduzi huo, mambo yalikuwa ni moto kwani mastaa mbalimbali waliibuka na burudani zilikuwa ni za kufa mtu.
Baadhi ya mastaa walioibuka ni muigizaji nguli Bongo, Kulwa Kikumba ‘Dude’, Blandina Chagula ‘Johari’, Salome Urasa ‘Thea’, David Genzi ‘Young Dee’, Abdulazizi Chende ‘Dogo Janja’ na mwanamuziki mwingine anayefanya vizuri kwa kasi na anajulikana kwa jina la Q Boy Msafi.
Hata hivyo mbali na wanamuziki hawa kutoa burudani na kuwasisitiza wakazi wa Tabata- Segerea kutumia juice maridhawa kutoka Kingdom, katika uzinduzi huo kila mtoto aliyekuwa maeneo hayo alipata juice bure.
Kwa upande wa Mkurugenzi wa Juice Kingdom, Zabron akizungumza na Wikenda alisema kwamba watengenezaji wa juice ni wengi lakini hakuna anayeshindana na Kingdom Juice.
“Unajua juice zetu ni za kiwango cha juu sana, tunazingatia afya ya mwanadamu na tunamuandalia kiliocho bora. Kwa watu wenye kufahamu lakini hawazingatii ni kwamba juice ni matunda, na matunda ni muhimu kwa afya ya binadamu.
“Sasa kuna watu unakuta kutokana na ubize wanashindwa kupata matunda wanayoyataka, sasa sisi Juice Kingdom tumewarahisishia watu, tunatengeneza juice za kila aina kwa hiyo badala ya mtu kuhangaika na matunda anaweza kupita akajipatia juis yake safi na maisha yakaendelea,” alisema Zabron.
Hata hivyo Zabron aliendelea kueleza kwamba tawi hilo la Tabata-Segerea ni moja kati ya matawi mengi ya Juice Kingdom na wanaendelea kuyafungua kutokana na namna watu wanavyofurahia juice za Kingdom.
Comments are closed.