The House of Favourite Newspapers

Maua Sama Afafanua Bifu Na Nandy

0

MSANII wa Bongo Fleva, Maua Sama, amefungukia kuhusu madai ya kuwa na tofauti na msanii mwenzake Faustina Charles ‘Nandy’.

 

Akizungumza na Risasi Vibes, Maua ambaye kwa sasa anatamba na ngoma ya ‘Kan Dance’ amesena kuwa yeye na Nandy hawana utofauti ila ni kwamba hawana ukaribu ndiyo sababu ya kutokuonekana pamoja kwenye baadhi ya matukio.“

Mimi mbona sina ugomvi wa aina yoyote tuko sawa kabisa, labda hii inatokana na kutokuonekana tukiwa pamoja kwenye kazi mbalimbali,” alisema Maua.Wawili hao wamekuwa wakidaiwa kuwa kwenye bifu la chini chini ambapo bifu hilo limejadiliwa zaidi mitandaoni.

Leave A Reply