The House of Favourite Newspapers

Mbeya City Yaitungua Simba Sokoine

0

MECHI ya Ligi kuu Tanzania Bara imemalizika katika Dimba la Sokoine jijini Mbeya huku Mnyama Simba akiambulia kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa Mbeya City.

 

Goli la Mbeya City limefungwa na mshambuliaji Paul Nonga dakika 20 , kwa upande wa Simba walikosa mkwaju wa Penati kupitia kwa Chris Mugalu.

 

Nahodha wa Mbeya city Mpoki Mwakinyuki alitolewa kwa kadi nyekundu katika kipindi chanza dakika ya 43 ya mchezo na kuwafanya kucheza pungufu mpaka mwisho wa mchezo.

 

Kwa matokeo hayo Simba imebaki na alama 24 bada ya kucheza michezo 11 huku Yanga ikiongoza ligi hiyo  alama 32.

Leave A Reply