Mbunge Nassari Anusurika Kuuawa Kwa Risasi Na Watu Wasiojulikana – Video
MBUNGE wa Jimbo la Arumeru Mashariki, Joshua Nassari usiku wa kuamkia leo yeye na familia yake walivamiwa nyumbani kwao na kundi la wahalifu wasiojulikana wakiwa na silaha na kufyatua risasi kama mvua kwa lengo la kumshambulia Mbunge huyo.
Hata hivyo kelele za mbwa na kutojua nyumba anayolala Nassari kati ya nyumba tatu zilizopo eneo hilo zimesaidia kumwokoa ambapo watu hao walifanikiwa kumuua mbwa wake mkubwa huku Mbunge huyo na mkewe wakifanikiwa kutoroka na kutokomea kizani usiku na baadaye kutoa taarifa Polisi.
Kabla ya tukio hilo, Mbunge Nasari mchana wa Ijumaa alitembelea wahanga wa tukio la kushambuliwa kwa mapanga kwa baadhi ya wananchi katika kata ya Makiba siku moja kabla ya marudio ya uchaguzi mdogo wa udiwani.