The House of Favourite Newspapers

Messi Amtumia Ujumbe Gaucho

Mshambuliaji wa Barcelona, Lionel Messi.

LIONEL Messi wa Barcelona amemtumia ujumbe nyota wa zamani wa timu hiyo, Ronaldinho ambaye amestaafu kucheza soka la kulipwa.

Ronaldinho.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Messi ambaye bao lake la kwanza alifunga akipata basi ya Ronaldinho ameandika ujumbe huu:

“Kama ambavyo nimekuwa nikisema, nimejifunza mengi kwako. Nitaendelea kukushukuru kwa kufanya mambo kuwa rahisi kwangu nilipojiunga na timu.

 

“Nilikuwa na bahati kuwa karibu yako, licha ya kuwa staa uwanjani lakini nje ya uwanja ulikuwa mtu mwema na hilo ndilo jambo muhimu, licha ya kuwa umeamua kustaafu, soka halitasahau tabasamu lako, nakutakia kila la kheri, Gaucho.”

Comments are closed.