Meya wa Jiji Dar Ahudhuria Kuagwa kwa ‘Bikira wa Kisukuma’ Leaders Club
MWILI wa marehemu Seth Katende ‘Bikira wa Kisukuma’, aliyekuwa mtangazaji wa kituo cha redio cha Efm, kipindi cha Ubaoni, umeagwa katika viwanja vya Leaders Club, jijini Dar es Salaam, ambapo baada ya kumalizika kwa shughuli hizo, safari ya kuelekea kwenye makazi yake ya milele, kwenye Makaburi ya Kinondoni ilianza na hatimaye maziko yamefanyika leo mchana wa Julai 12, 2017.
(PICHA: AMANI MADEBE, HILALY DAUDI | GLOBAL TV ONLINE)