The House of Favourite Newspapers

Miaka Miwili Kifo cha Mumewe… Mke wa Filikunjombe Aandika Ujumbe Mzito

0
Aliyekuwa Mbunge wa Ludewa, Deo Haule Filikunjombe (enzi za uhai wake) akiwa na familia yake.
IKIWA ni miaka miwili imepita sasa tangu aliyekuwa Mbunge wa Ludewa, Deo Haule Filikunjombe afariki dunia, mke wa wake Sarah Habiba amesema Tanzania ina pengo kubwa kwa kumpoteza Deo.
 
Kwenye ukurasa wake wa instagram, Sarah Habiba ameandika ujumbe huo, huku wakiadhimisha miaka miwili ya kifo chake kwa kufanya ibada takatifu.
 
“Mume wangu leo umefikisha miaka miwili tangu upatwe na mauti, kiukweli umeacha pengo kubwa kwa watanzania, jamii na familia kiujumla, watoto wako wanakumiss sana, mimi mkeo, Mungu akulaze mahala pema peponi mpenzi wangu, ntakukumbuka daima mpenzi”, aliandika  jana Sarah Habiba.
Ujumbe alioandika mke wa Filikunjombe.
 
Deo Filikunjombe alifariki Octoba 15, 2015 kwa ajali ya helkopta iliyoanguka kwenye msitu wa hifadhi ya Selous akitokea Dar es salaam kwenda Ludewa, akiwa na rubani wake William Silaa ambaye ni baba mzazi wa Jerry Silaa, na msaidizi wa Deo Filikunjombe, Bwana Mkwera ambao pia walifariki dunia.
 
Deo Filikunjombe atakumbukwa kwa uchapa kazi wake na juhudi alizozionyesha kwenye kamati ya Bunge kuibua sakata la Escrow akiwa na wabunge wengine, akiwemo rafiki yake wa karibu mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe.

Kauli ya Mwigulu:Wanaoingia Nchini Bila ya Kufuata Taratibu za Tanzania

Leave A Reply