Mimi Mars; Ndugu, marafiki walimuogopa kwa umbeya
MSANII anayekuja kwa kasi katika gemu la muziki Bongo, Mariane Mdee ‘Mimi Mars’ amefunguka kwamba enzi za utoto wake alikuwa na tabia ya umbeya, hali iliyosababisha ndugu zake akiwemo dada yake Vanessa Mdee ‘Vee Money’ kumkwepa.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda, Mimi Mars ambaye kwa sasa anatamba na kibao chake cha Kodoo alisema zamani alikuwa na tabia ya kuongeaongea hovyo kiasi cha kuwakera wengi lakini anashukuru Mungu alivyokua hiyo tabia akaachana nayo.
“Kweli ukiwa na utoto unakuwa na mambo mengi lakini ukikua unaacha, tabia yangu ya uropokaji na umbeya vilinifanya niogopwe. Yaani nikiwa nimekaa sehemu watu wananikwepa lakini najua ilikuwa utoto tu, sasa nimekuwa nimeacha,” alisema Mimi Mars.
Mimi Mars alidai kuwa kitendo hicho kilikuwa kinamkera sana Vanessa na baadhi ya ndugu zake ambao ilifikia kipindi wakiwa wanaongea mambo yao wanamfukuza kwani walikuwa wanajua atakachofanya.
Stori: Memorise Richard.
Comments are closed.