The House of Favourite Newspapers

Mjane wa Kobe Bryant Alipwa Dola Milioni 16 baada Picha za Mumewe Kuvujishwa

0

BAADA ya picha za mwili wa aliyekua nyota wa mpira wa kikapu  wa Marekani Kobe Bryant kuvujishwa na naibu afisa wa polisi  ambaye alisambaza picha hizo kwenye mitandao. Hivyo mahakama imeamuru Mke wa marehemu Kobe alipwe dola milioni 16 kama fidia kutokana na kuvuja kwa picha hizo.

Mke wa Kobe Bryant Bi Vanessa Bryant

Mke wa wa Kobe Bi Bryant alitoa ushahidi huku akibubujikwa na  machozi wakati wa kesi hiyo katika siku 11 alisema kwamba habari za picha hizo zilizidisha huzuni yake baada ya kumpoteza mumewe na bintiye kwenye ajali hiyo iliyotokea 2020.

Marehemu kobe Bryant Na Gianna Bryant enzi za uhai wao

Alipokua akishuhudia kuhusu tukio hilo amesema tukio hilo limemfedhehesha sana na kumfanya aingiwe na uoga,picha hizo zilionyesha mwili wa marehemu kobe.

 

“Nilihisi kutaka kukimbia na kwenda kujitupa kwenye maji na kupiga kelele, tatizo siwezi kukataa uhalisia wangu  siwezi kuukimbia mwili wangu” alisema Bi Bryant

 

Imeandikwa: Dunstan Mtili Erick kwa msaada wa Mitandao

Leave A Reply