The House of Favourite Newspapers

Mkurugenzi Wa Ilemela, Mwanza Akanusha Taarifa Za Wanawake Kujifungua Sakafuni

0

OFISI ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela mkoani Mwanza imekanusha taarifa za wanawake kujifungua sakafuni katika kituo cha afya cha Buzurugwa mkoani Mwanza.
Taarifa ya mkurugenzi wa halmashauri hiyo imeeleza kuwa awali kulikuwa na vitanda vitatu kwa ajili ya wanawake kujifungulia, baada ya ongezeko la mahitaji serikali ilongeza vitanda vitatu na kuwa sita.
Wakili Kiomoni Kibamba amesema sambamba na hilo serikali ilijenga jengo la mama na mtoto lenye uwezo wa kulaza akina mama 42 lenye thamani ya Sh milioni 200 fedha za ndani za halmashauri.

Leave A Reply