Msanii wa Filamu Elizabeth Michael ‘Lulu’ Afunguka Kumtuliza Mzazi Mwezie Majizo
Msanii wa Filamu nchini Elizabeth Michael ‘Lulu’ amefunguka kilichosababisha kumtuliza mzazi mwezie, Francis Ciza maarufu kama Majizo.
Akizungumza na IJUMAA hivi karibuni mwanamama huyo amesema kuwa kwenye uhusiano wao misingi ya ukweli na utofauti ndiyo imewafanya hadi sasa wapo pamoja.
“Kitu ambacho nimefanya hadi kuweza kutulia na mume wangu baba G ni misingi ya kuwa ‘real’, kingine labda kuna vitu tofauti ameviona kutoka kwangu ndiyo maana nimetulia,” alisema Lulu.
STORI:KHADIJA BAKARI