WINGA wa Klabu ya Difaa El Jadida ya Morocco, Simon Msuva leo Jumatatu ametoa msaada katika Kituo cha Kulelea Watoto wenye mahitaji maalumu cha Ijango Zaidia kilichopo Sinza Madukani jijini Dar.
Msuva ambaye aliwika na Yanga kabla ya kwenda Morocco amesema: “Nimeamua kutoa hiki kidogo ambacho nimekichuma Morocco kwa Watanzania wenzetu, hawa ni binadamu wenzetu ambao wanahitaji huduma kama watu wengine.”
Msuva alikabidhi vitu hivyo kama mchele, sabuni za kuogea, mafuta ya kupikia, vinywaji na vitu vingine mbalimbali.
Naye Mkurugenzi wa kituo hicho cha Ijango Zaidia, Zaidia Nuru amesema: “Tunashukuru kwa msaada huu ambao tumepata kutoka kwako, kwa uwezo wa Mungu tunaomba akuongezee zaidi ya hiki ambacho umetupa.”
HABARI/PICHA: MUSA MATEJA/GPL.
Comments are closed.