The House of Favourite Newspapers

Mume Akana Kumpiga Mkewe, Afichua Siri Nzito – ”Kapigwa Na Mchepuko, Alikuwa Anatembea Na Mjomba”-Video

0

Mapya yameibuka katika sakata la mwanamke Jackline Mkonyi kudai amepigwa, kung’olewa meno na kutobolewa jicho na mumewe ambapo mwanaume anayetuhumiwa, Isaack Mnyagi ameibuka na kudai kwamba siyo yeye aliyempiga mkewe bali amepigwa na mwanaume wake mwingine (mchepuko).

Akizungumza kwa njia ya simu na Global TV, mwanaume huyo amesema mkewe huyo amekuwa na tabia ya kuwa na uhusiano na wanaume wengi nje ya ndoa yao, huku akitoa madai mazito kwamba pia amekuwa na uhusiano wa kimapenzi na mjomba wake.

Wakati mwanaume huyo akijieleza kwa upande wake, Jackline yeye anadai kwamba ni mumewe ndiye aliyemfanyia ukatili huo na kwamba tayari walisharipoti polisi, kauli ambayo pia imeungwa mkono na baba wa mwanamke.

Leave A Reply