The House of Favourite Newspapers

Mume Amuua Mkewe Kisha Kujinyonga

0

Edward Manyangu (41) Mkazi wa Wilaya ya Busega anadaiwa kumuua Dalali Maunga (41) kwa kumpiga na kitu kizito kichwani baada ya kutokea Ugomvi ambapo Mwanaume alimtuhumu Mkewe kuwa na uhusiano nje ya Ndoa.

 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu, Richard Abwao, amesema baada ya kutekeleza mauaji hayo, Manyangu alijiua kwa kujinyonga kwa kamba aliyofunga kwenye Mti ulioko nje ya nyumba yao.

 

Kwa mujibu wa ujumbe wa maandishi unaoaminika kuandikwa na Manyangu, alikuwa akimtuhumu Mkewe kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Mwanaume mwingine.

 

Leave A Reply