The House of Favourite Newspapers

Mume wa Shilole Aukana Usangoma

Mwanamuziki Zuwena Mohammed ‘Shilole’ akiwa na mume wake Ashrafu Uchebe.

MUME wa mwanamuziki Zuwena Mohammed ‘Shilole’ Ashrafu Uchebe amekana kuwa mganga (Sangoma) wa kutumia vitabu na kuweka wazi kuwa kazi yake ni ufundi wa magari.

 

Maelezo hayo yamekuja kutokana na madai yaliyokuwa yumeenea kwamba, mbali na kufanya mambo mengine lakini pia anatibu kwa kutumia Quran na amekuwa akifanya hivyo tangu alipokuwa Zanzibar.

Akizungumza na Risasi Jumamosi, Uchebe alifunguka hivi: “Kama unavyojua kumuombea mtu dua ni jambo la kawaida lakini anayesaidia ni Mungu, hata wewe nakuombea tu dua na Mungu ndiye anasaidia ila hilo la kuwa mganga sijawahi, kazi yangu ni fundi wa magari,” alisema Uchebe

Comments are closed.