The House of Favourite Newspapers

Mvutano wa Rwanda Vs Uganda Mpaka Wafungwa

Serikali ya Uganda imemtaka Balozi wa nchi ya Rwanda nchini humo Meja Jenerali Frank Mugambage kueleza mvutano wa kidiplomasia kuhusu sintofahamu kati ya mpaka wa nchi hizo jirani.

 

Uganda pia inamtaka Balozi wake nchini Rwanda kupata maelezo ni kwanini mvutano huo unaendelea kushuhudiwa.

 

Hali ya wasiwasi imeshuhudiwa wiki hii baada ya serikali ya Rwanda kufunga mpaka wa Gatuna kwa kile ilichosema kuwa, ulikuwa unakarabatiwa na kulazimu magari ya mizigo kutoka Uganda kupitia mpaka mwingine wa Kagitumba, umbali wa Kilomita 114.

 

Serikali ya Rwanda, imewataka raia wake wanaokwenda nchini Uganda kuwa makini, kwa madai kuwa raia wake wanakamatwa na kurudishwa nyumbani kwa nguvu.

Comments are closed.