MWAMUNYANGE AKABIDHI KOMBE FAINALI ZA TULIA CUP TUKUYU MBEYA
Mkuu wa Majeshi Mstaafu, Davis Mwamunyange amekabidhi kombe kwa timu ya Ndanto FC, baada ya kushika nafasi ya kwanza kwenye michuano ya Tulia Cup 2017.
Michuano hiyo ilifanyika kwenye Uwanja wa Tandale Tukuyu wilayani Rungwe mkoani Mbeya. Vodacom ndiyo walikuwa wadhaminiwa wakuu wa michuano hiyo. Katika mchezo huo Ndanto walishinda kwa mabao 2-1 na kutwaa kombe hilo kwa mwaka huu 2017 na kitita cha sh. milioni 1.5.