MWANAMUZIKI WALID ALIVYODATISHA WABONGO MASAKI DAR
MWANAMUZIKI wa Kibongo aliyekuwa akifanyia kazi ya muziki nchini Uholanzi, Walid Ali, ambaye anabamba na vibao vya Dunia na Ni Wewe, usiku wa kuamkia leo amefanya pati ya kurudi rasmi nchini ambayo ilifanyika Klabu ya Paparazzi iliyopo Masaki Jijini Dar.
Walid alisema sasa amehamishia rasmi kazi yake hiyo hapa nchini baada ya kumaliza masomo yake Uholanzi.Katika pati hiyo Walid aliudatisha umati uliofurika kwenye klabu hiyo ambapo madada walionekana kubanjuka kwa staili ya chura kutokana na mdundo uliokuwa ukiporomoshwa
HABARI/PICHA: RICHARD BUKOS / GPL
Comments are closed.