Waombolezaji wakisaidia kubeba mwili wa marehemu kwa ajili ya maziko.
Taswira ya msibani.
Waandishi, Denis Mtima na Hamida Hassan wakimfariji mfiwa, Mayasa Mariwata.
MWANDISHI wa habari wa magazeti pendwa ya Global Publishers Ltd , Mayasa Mariwata amepata pigo la kufiwa na baba yake mzazi, Amiry Mariwata ambaye amefariki mapema jana baada ya kuzidiwa na kisukari akiwa nyumbani kwake Kinondoni jijini Dar.
Mwili wa marehemu umezikwa leo katika makaburi ya Mwananyamala baada ya sala ya Adhuhuri.
Global Publishers inawapa pole wafiwa wote wa familia hiyo kwa kipindi hiki kigumu.
“Inalillah Waina Ilaih Rajiun”
Picha/ Chande Abdallah