MWANZA: MPWA WA SHIGONGO AUVUA UKAPELA
MPWA Wa Mkurugenzi Mtendaji wa Global Group Ltd aitwaye, Emmanuel Aron, wa Jijini Mwanza leo amefunga pingu za maisha na mrembo, Christina John.
Ndoa hiyo imefungwa katika kanisa la Familia Takatifu Nundu-lililopo Meco Jijini Mwanza huku ibada ya harusi hiyo ikiongozwa na Padri Moses Mapera.
Katika mahubiri yake Padri amewaasa wanandoa hao kuwa watu wenye kuheshimiana, kuombeana msamaha pale wanapokesea ili waweze kufurahia ndoa yao.
Alisema kuwa kama wanandoa hao wataheshimu misingi yote ya harusi ikiwemo upendo na mambo mengine ndoa hiyo itakuwa imara milele na milele.
Amewataka wanandoa hao kushirikiana katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo ili familia hiyo iweze furahia maisha kama mungu anavyopendezwa.
Comments are closed.