MWANZA: WASAFI WAANGUSHA BONGE LA PARTY, DUDU BAYA AIBUKA NA KIFAA
Kundi la Wasafi Classic Baby (WCB) katika kuonesha wameikamia shoo yao ya Wasafi Festival inayotarajiwa kufanyika leo Jumamosi usiku wa kuamkia leo wameangusha bonge la Pre Party kwenye Ufukwe wa Jembe ni Jembe jijini Mwanza.
Crew ya Wasafi waliwasili jijini humo jana wakiongozwa na mwanamuziki, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.
Katika hafla hiyo ya jana usiku, baadhi ya mastaa waliyokuwepo ni Diamond mwenyewe, Lavalava, Young Killer, Gigy Money, Wolper, Chin Bees, Dudu Baya na wengine.
Mashabiki Wamvamia DIAMOND Hotelini Mwanza ”WASAFI FESTIVAL”
Mashabiki wa Jiji la Mwanza leo Jumamosi ya Desemba 15, 2018, watashuhudia Bonge la Shoo kutoka kwa WCB katika Uwanja wa CCM Kirumba.
PICHA: RICHARD BUKOS / GPL- MWANZA
Comments are closed.