MWANAMKE Mzungu anayejulikana kwa jina la Monique Honsbeek anayedaiwa kufanya ukahaba katika Jiji la Dar es Salam leo amefikishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Victoria Nongwa na kusomewa shitaka moja la kuishi nchini bila kibali.
Mtuhumiwa amekana shitaka hilo na akatakiwa kusaini bondi ya dhamana ya Sh. milioni moja na wadhamini wawili wa Tanzania. Kesi yake imeahirishwa hadi Septemba 27 mwaka huu.