Dkt. Mary Mwanjelwa (kushoto) akiwa na baadhi ya wahitimu wenzake.
NAIBU Waziri Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Mary Mwanjelwa, amewahimiza wafanyakazi kote nchini kujiendeleza kielimu ili kufikia malengo yao.
Kauli hiyo ameitoa jana wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya kufanyika mahafali ya 37 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania eneo la Bungo, Kibaha Mkoa wa Pwani wakati alipokuwa akitunukiwa Shahada ya Uzamivu (PhD).
Katika mahafali hayo, mgeni rasmi alikuwa rais mstaafu wa awamu ya nne, Jakaya Mrisho Kikwete.