The House of Favourite Newspapers

NANDY AFUNGUKIA MADAI YA UJAUZITO

Faustine Charles ‘Nandy’

MREMBO anayefanya vizuri kunako Muziki wa Bongo Fleva, Faustine Charles ‘Nandy’ amefungukia madai ya kuwa na ujauzito wa kigogo mmoja na kusema kuwa ni uzushi tu siyo kweli.  Akizungumza na Risasi Vibes, mrembo huyo alisema watu huwa wanaamua tu kuzusha mambo yasiyokuwa na ukweli wowote ule ndani yake, ili mradi tu wafurahishe mioyo yao kitu ambacho kinaumiza.

“Hizo tetesi zinazosambaa mitandaoni kwamba nina mimba siyo za kweli, ila naona watu wameamua tu kuzizusha ili wafurahishe mioyo yao, sina mimba jamani naomba waniache,” alisema Nandy.

Stori: MEMORISE RICHARD

Comments are closed.