Ndoa ya Meneja wa Global Publishers, Abdallah Mrisho Yatikisa Dar (Video)
Meneja wa Global Publishers, Abdallah Mrisho, jana (Jumamosi, Sept. 30,2017) alifunga ndoa ya kifahari na Catherine Mdami, iliyolifanya Jiji la Dar es Salaam lisimame kwa muda kutokana na maandalizi yake bab’kubwa, ikifuatiwa na sherehe ya kukata na shoka iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mlimani City.
Katika sherehe hiyo ambayo MC alikuwa ni mtangazaji wa Clouds TV, Harris Kapiga, wafanyakazi wa Kampuni ya Global Publishers wakiongozwa na mkurugenzi wao, Eric Shigongo, ndugu, jamaa na marafiki, walijumuika kula, kunywa mpaka kusaza na kucheza muziki mzuri, mpaka usiku sana huku kukiwa na ‘special appearance’ ya Mbunge wa Mtama, Mhe. Nape Nnauye na msanii wa Bongo Movie, Jackline Wolper.
Kwa upande wa burudani, Bendi ya Banana Zorro (B-Band), ikiongozwa na Banana mwenyewe pamoja na msanii wa kitambo kwenye muziki wa kizazi kipya, Nuruely, iliangusha burudani ya nguvu, ikipiga ‘cover’ ya nyimbo mbalimbali zilizowaburudisha vilivyo waliohudhuria.