Ndugai Apendekezwa Spika wa Bunge,Tulia Naibu
Kamati Kuu ya Halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM ambayo iliketi jana Dodoma imempongeza Rais John Magufuli kwa kushinda kiti cha urais kwa muhula wa pili ya mwaka 2020-25.
Pia imewapendekeza Job Ndugai kuwania nafasi ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Dkt. Tulia Ackson kuwania Naibu Spika na Zuber Alli Maulid kuwania Spika wa Baraza la Wawakilishi.