The House of Favourite Newspapers

NECTA Yawafutia Matokeo Wanafunzi 10 wa Kidato cha Sita

1

 

Wakati matokeo ya mitihani ya kidato cha sita yakitolewa leo, Jumamosi Julai 15, imebainika kuwa watahiniwa 10 walifutiwa matokeo kwa makosa ya kufanya udanganyifu.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa (Necta),  Dk Charles Msonde imeeleza kuwa kati ya watahiniwa hao kumi, saba ni wa shule na watatu ni wa kujitegemea.

Matokeo Ya Kidato Cha Sita Yatangazwa, Bofya Hapa Kuyaona

Pamoja na hao kumi, matokeo ya watahiniwa wengine 15 yalizuiliwa kwa kuwa hawakufanya mitihani ya baadhi ya masomo.

Watahiniwa hao walishindwa kufanya mitihani kutokana na matatizo mbalimbali ikiwamo ya kiafya na hivyo kushindwa kufanya baadhi ya mitihani hiyo.

Vinara wa Matokeo Kidato cha Sita Hawa Hapa

‘Watahiniwa hao wamepewa fursa ya kufanya mitihani ya kidato cha sita, Mei 2018 kama wa watahiniwa wa shule,” imesema taarifa ya Dk Msonde.

Pia, wapo watahiniwa 69 wa shule ambao walipata matatizo ya kiafya na kushindwa kufanya mitihani yote, wamepewa fursa ya kufanya mitihani hiyo, Mei 2018.

 

 

TOVUTI YA BARAZA LA MITIHANI TANZANIA (NECTA)

MATOKEO KIDATO CHA SITA (ACSEE) 2017

MATOKEO YA DIPLOMA YA UALIMU (DSEE) 2017

MATOKEO YA CHETI CHA UALIMU (GATCE) 2017

1 Comment
  1. […] NECTA Yawafutia Matokeo Wanafunzi 10 wa Kidato cha Sita […]

Leave A Reply