The House of Favourite Newspapers

NEYMAR AWEKWA NJE YA UWANJA PSG, HOFU YATANDA

0

Mshambuliaji Neymar huenda akaukosa mchezo wa timu yake ya PSG itakapopambana dhidi ya Montpellier kutokana na kudaiwa kuwa na majeraha madogo ya mguu.

Klabu hiyo imeamua hiyo ili kumpa muda wa kumpumzika kabla ya kukutana na Bayern Munich katika Ligi ya Mabingwa Ulaya, wiki ijayo.

PSG yenyewe itacheza wikiendi hii katika mwendelezo wa Ligue 1 lakini klabu hiyo imeamua imuweke staa huyo pembeni kutokana na hofu ya kuumia na kuukosa mchezo huo ujao dhidi ya Bayern.

Tangu aanze kuichezea PSG hivi karibuni, Neymar amefunga mabao mane na kutoa asisti nne.

Leave A Reply