The House of Favourite Newspapers

Ngoma, Kamusoko Warejea Kuipa Ubingwa Yanga SC

BAADA ya juzi Jumamosi, timu ya Yanga kufanikiwa kuifunga Azam FC mabao 2-1, habari njema kwa wapenzi na mashabiki wa timu hiyo ni kwamba, muda wowote kuanzia leo, mshambuliaji wa kutumainiwa wa timu hiyo, Mzimbabwe, Donald Ngoma atarejea uwanjani baada ya kupona majeraha yake yaliyokuwa yakimsumbua.

 

Ngoma amekuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu na kushindwa kuitumikia timu yake hiyo ya Yanga kutokana na kusumbuliwa na nyonga aliyoumia Septemba 30, mwaka jana wakati  ilipokuwa akiitumikia timu hiyo dhidi ya Mtibwa Sugar katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

 

Kukosekana kwa Ngoma timu hiyo kupunguza makali yake katika safu ya ushambuliaji, jambo ambalo hiyo. Akizungumza na Jumatatu, Mwenyekiti wa ya Yanga, Hussein Nyika, alisema kuwa Ngoma hivi sasa yupo fi ti na alikuwa akiendelea na stamina katika moja ya gym zilizopo jijini Dar es Salaam na programu yake hiyo ilimalizika jana Jumapili.

 

“Kwa hiyo muda wowote kuanzia leo, Ngoma ataanza kufanya mazoezi ya uwanjani pamoja na wachezaji wenzake.

 

“Hakika hiyo ni habari njema sana kwetu na imeturudishia matumaini yetu kuwa sasa tunaweza kutetea ubingwa wetu, kwani hata Thabani Kamusoko naye tayari ameshapona na Mungu la FA dhidi ya Ihefu anaweza akapewa nafasi ya kucheza,” alisema Nyika.

 

Sweetbert Lukonge, Dar es Salaam   

Comments are closed.