The House of Favourite Newspapers

 Poshy ahofia kuvunja ndoa za watu

AMA kweli siku hizi mastaa wameelimika, mrembo mwenye kusumbua jiji kutokana na umbo lake, Jacqueline Obeid ‘Poshy Queen’ amesema anamuomba Mungu amuepushe asinase kwenye mapenzi na waume za watu.

Akizungumza na Amani, Poshy alisema anamuomba Mungu asimuingize kwenye mtego huo kwa sababu anaamini atatenda dhambi mbaya ya kuvunja ndoa ya mtu bila sababu.

“Kitu ambacho namuomba Mungu kila siku ni kuniepusha na dhambi ya kutembea na mume wa mtu kwa sababu najua wazi nikiingia tu, naweza kuivunja ndoa kitu ambacho siyo kizuri kabisa na pia Mungu hapendi,” alisema Poshy.

Stori: Imelda Mtema

Comments are closed.