The House of Favourite Newspapers

POSHY ATOA SIRI YA KUOGOPWA NA WANAUME

Jacqueline Obed ‘Poshy Queen’

MREMBO ambaye ametengeza jina lake kupitia umbo lake ‘matata’, Jacqueline Obed ‘Poshy Queen’ amefunguka kuwa, moja ya silaha kubwa ya warembo kuogopwa na wanaume ni kufanya kazi.

 

Akizungumza na Showbiz Xtra, Poshy ambaye amefungua duka lake la nguo za ndani linaloitwa Poshy Secret lililopo, Sinza-Palestina, amesema kuwa staa yeyote akiwa mzuri halafu akafanya kazi anazidi kung’ara na hata wanaume wanamugopa wanajua wazi kwamba, si mwanamke wa mchezomchezo.

 

“Unapokuwa staa na ukaamua kufanya kazi basi itakuwa dawa moja kubwa sana ya kukulinda na wanaume, lazima watakuogopa; utaheshimika na kisha uzuri wako utaonekana mara dufu,” alisema Poshy.

Comments are closed.