Prof. Jay Amtambulisha Mkewe Kwa Wapiga Kura Wake Mikumi
MBUNGE wa jimbo la Mikumi Joseph Haule Profesa Jay leo yupo jimboni kwake Mikumi kwa ajili ya kusherehekea ndoa yake na wananchi wa jimbo lake baada ya wiki iliyopita kufunga pingu za maisha katika kanisa la St Joseph jijini Dar es Salaam.
Katika kuonyesha ni namna gani ana mapenzi na wapiga kura wake wa Mikumi, leo ameamua kufanya sherehe nyingine baada ya ile ya Mlimani City Dar.
Profesa Jay anafanya sherehe hii ya wazi kwenye uwanja wa Bustani na wakati stori hii inaandikwa kuna gari zima la Coca Cola ambalo lipo mahususi kwa ajili ya kuwagawia soda wakazi wote wa Mikumi waliojitokeza uwanjani hapa.
Mbali na soda, Jay amewaandalia chakula cha kutosha ambacho wote watakaotaka kujumuika naye watakula kadiri wawezavyo.
PICHA: MUSA MATEJA | GLOBAL PUBLISHERS | MIKUMI – MOROGORO