The House of Favourite Newspapers

Profesa J Kuuaga Ubachela Karibuni

0

 

MBUNGE  wa Jimbo la Mikumi kupitia tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambaye pia ni mwanamuziki wa Hip Hop  hapa Bongo, Joseph Haule maarufu kwa jina la Profesa Jay,  anatarajia kuuaga ukapela kwa kufunga ndoa na mpenzi wake wa muda mrefu anayefahamika kwa jina la Grace Mgonjo.


Profesa Jay ambaye ametamba sana na kibao chake cha ‘Kazi Kazi’  alichomshirikisha  msanii wa singeli Sholo Mwamba, yuko kwenye maandalizi ya ndoa ambapo tayari send off imekwishafanyika.

Na Isri Mohamed, (GPL)

 

Leave A Reply