The House of Favourite Newspapers

Quick Rocka: Penzi la Kajala halinitesi

0

Kajala-na-QuickQuick Rocka na Kajala Masanja.

Stori: Boniphace Ngumije

MSANII anayekimbiza katika Tasnia ya Muziki wa Bongo Fleva, Quick Rocka amedai kuwa penzi la muuza sura kwenye Filamu za Kibongo, Kajala Masanja halimtesi maana ni la kishkaji na kila mmoja kati yao ana uhuru wa kufanya mambo yake binafsi kutokana na matakwa yake bila kumbana mwenziye.

Akipiga stori na safu hii ya burudani Quick ambaye kwa sasa ameachia ngoma mpya iitwayo Hapo aliyomshirikisha G Nako alisema, tofauti na watu wengi waliyoko kwenye mapenzi wanaokuwa wanabanwa na wapenzi wao katika shughuli za kawaida kwa ajili ya kujitafutia kipato, kwake haiko hivyo, yeye na Kajala wamepeana uhuru.

“Sijui nikweleze vipi kuhusu penzi langu na huyo diva, wewe elewa tu liko kishkaji, kila mtu ana uhuru wa kufanya mambo yake na haina kubanana, hata hivyo wakati mwingi ninakuwa naye,” alisema Quick Rocka.

Alipoulizwa juu ya tetesi zinazosambaa za Kajala kutoka na msanii wa Bongo Fleva, Msami alisema hajui chochote kuhusu wawili hao.

KUNUNUA NA KUSOMA MAGAZETI YA GLOBAL PUBLISHERS ONLINE, INGIA HAPA==>VODACOM M-PAPER APP

*********

JIUNGE NA SOCIAL MEDIA ZETU:

KWA HABARI ZA KITAIFA, KIMATAIFA, MASTAA NA MIKASA YA KUSISIMUA

INSTAGRAM: @Globalpublishers

TWITTER: @GlobalHabari

FACEBOOK: @GlobalPublishers

SUBSCRIBE YOU TUBE: GlobalPublishers

GLOBAL TV ONLINE: www.globaltvtz.com

HADITHI ZA KUSISIMUA NA MBINU ZA UJASIRIAMALI, ERIC SHIGONGO FACEBOOK PAGE: @shigongotz

Leave A Reply