The House of Favourite Newspapers

Rais Magufuli Amtuma Kikwete Zimbabwe

 

Rais Dkt. John Magufuli amemtuma Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Dkt. Jakaya Kikwete kumwakilisha katika sherehe za uapisho wa Rais mteule wa Jamhuri ya Zimbabwe, Emmerson Mnangagwa zitakazofanyika kesho mjini Harare.

 

Mnangagwa ataapishwa kesho kuongoza nchi ya Zimbabwe baada ya kushinda katika uchaguzi Mkuu uliofanyika Julai 30 akiwa amepokea kijiti kutoka kwa aliyekuwa Rais wa nchi hiyo, Robert Mugabe.

 

Emmerson Mnangagwa alitangazwa na Tume ya Uchaguzi nchini Zimbabwe kuwa mshindi wa kiti cha Urais kwa kupata jumla ya kura milioni 2.5 sawa na asilimia 50.8 katika uchaguzi huo ambapo mpinzani wake wa karibu, Nelson Chamisa wa Chama cha MDC amepata jumla ya kura milioni 2.15 sawa na asilimia 44.3 ya kura zote alizopigiwa na wananchi wa Zimbabwe.

Comments are closed.