JPM Apokea Ripoti ya CAG Ikulu, Dodoma (Picha +Video)
RAIS John Magufuli leo Machi 26, 2020, amekabidhiwa Ripoti ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali kwa mwaka 2018/2019 iliyowasilishwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere, katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu, Chamwino, jijini Dodoma.
Pia amepokea Ripoti ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) ya mwaka 2018/2019 iliyowasilishwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi hiyo Brigedia Jenerali John Mbungo.
PICHA NA IKULU