Rais Samia Ateua Wawili
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan leo Septemba 20, amefanya uteuzi wa viongozi wawili.
Rais Samia Amemteua Bw. Yona Killagane kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama Vya Ushirika-COASCO.
Pia Rais Samia amemteua Mathew Modest Kirama Kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma-PSC, uteuzi huo umeanza Septemba 18, 2021.