Rais Samia Suluhu Hassan ameanza ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani Morogoro kuanzia Julai 7, 2021. Akiwa mkoani humo, pamoja na mambo mengine atazungumza na wananchi na kuhudhuria mkutano mkuu wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) unaofanyika leo Julai 8.