Rais Samia Awatakia Pasaka Njema Watanzania Wote
Leo Aprili 4 Wakristo ulimweguni kote wanaadhimisha kufufuka kwa Yesu Kristo (sikukuu ya Pasaka ,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kupitia ukurusa wake kwenye mtandao wa Twitter amewatakiwa pasaka njema watanzania wote.
“Nawatakia watanzania wote Pasaka njema, tuadhimishe ufufuko wa Yesu Kristo huku tukiliombea Taifa letu la Tanzania kudumisha amani, upendo na mshikamano. Tuendeleze jitihada za kuijenga nchi yetu kwa kuchapa kazi kwa juhudi na maarifa. Yesu amefufuka, Haleluya Haleluya.” – Rais Samia Suluhu