Rais Samia: Vijana Wengi Wanahangaika na Supu ya Pweza, Vumbi la Kongo -Video
RAIS Samia leo Ijumaa Septemba 30, 2022 ameagiza kufanyika utafiti wa kwanini vijana balehe wanamatizo ya lishe ili kuepuka kuwa na Taifa goigoi. Samia ameyasema hayo wakati wa hafla ya utiaji saini mkataba wa usimamiaji shughuli za lishe.
Amesema wakati wakutafuta watoto vijana hao wanahangaika mara kunywa supu ya pweza na kwamba kuna tatizo ambalo wanalijua lakini wanalificha.
“Watafiti fanyeni tafiti, tuna tatizo, kwasababu halisemwi ni siri linawaumiza zaidi vijana wetu, mara haya ninayoyataja, mara vumbi la Kongo, mara kitu gani lakini tatizo kubwa liko kwenye lishe. Sasa watafiti fanyeni tafiti vijana wetu waweze kuzaa watoto wenye afya,”amesema Rais Samia.
Amesema jamii hiyo ni ya watu wote waweze kufanyia kazi na kwamba wakiacha hilo liendelee wanaenda kuwa na Taifa goigoi ambalo lina watu lakini si raslimali watu ambao ni mzigo kwa Taifa na si wazalishaji kwa ajili ya Taifa.
“Tutafika mahali hatujui mume nani, mke nani. Kwa hiyo twendeni tukasimamie hilo…Wavulana mnaonekana mmevaa suti lakini kuna vigenge vya udongo (vumbi) la kongo chungu mzima, Amos (Mkuu wa Dar es Salaam-Amos Makala) unanitazama huko ndio kunasifika kwa chipsi,”amesema