The House of Favourite Newspapers

RANALDO: ANATAJWA BORA ZAIDI UEFA KIHISTORIA

MADRID, Hispania: MIEZI kadhaa iliyopita, kuna wengi waliombe­za Cristiano Ronaldo wakati akipitia kipindi kigumu cha ukame. Ni Ronaldo huyo­huyo ambaye aliibuka ghafla na kwenda kuipa Real Madrid ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Ulaya na La Liga.

Msimu huu pia, Ronaldo, 33, aliuanza kwa tabu, wengi wakaanza kuibua mas­wali tena juu ya kiwango chake, la­kini baada ya muda hakuna anaye­hoji tena.

 

Lakini ukweli ni kwamba huenda kizazi hiki tunamshuhudia mcheza­ji bora zaidi wa wakati wote katika Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Mashabiki Jumanne iliyopita kwenye Uwanja wa Juventus, wal­ishuhudia kila kitu kwa uwazi zaidi. Baada ya Ronaldo kupiga bao la pili kali (Real ilishinda 0-3 ugenini), i l i b i d i mashabiki wa upinzani wasimame tu kumpa heshima kutoka­na na jinsi bao hilo lilivy­okuwa.

 

“Sikuamini. Nalazimi­ka kusema asante kwa mashabiki wote wa Ju­ventus. Walichokifanya kwangu kinashangaza. Hii haijawahi kutokea katika maisha yangu,” alisema Ro­naldo, baada ya mashabiki wa Juventus kusimama na kumpongeza kufuatia bao kali aliloifunga timu yao.

Suala la mchezaji bora za­idi litaendelea kuwa mjadala milele kwa kuwa ni mtazamo wa mtu. Kila mtu huwa na chaguo lake; mweupe au mweusi? Chapati au mandazi? Vitumbua au sambusa? Kunyoa au kufuga rasta?

Lakini kwa kile ambacho alikifan­ya Ronaldo Jumanne, inawezeka­na wengi wakaanza kukubali kuwa huyu ni mchezaji mkali zaidi kihistoria katika michuano hii.

Takwimu zinambeba: Yeye bin­afsi tangu aondoke kwenye Premier, amefunga mabao mengi kwenye michuano hiyo kuliko jumla ya ma­bao yaliyofungwa na timu mbili za Manchester United na Manches­ter City.

 

Kumbuka huyu ndiye mfungaji bora wa wakati wote wa michua­no hii, akiwa na mabao 120.

Bao lake la ‘tiki taka’ Ju­manne, linasadikika kuwa ni bao bora zaidi lililowahi kufungwa katika historia ya mtoano wa Ligi ya Mab­ingwa. Lilifungwa dhidi ya mmoja wa makipa bora zaidi wa wakati wote duniani, na lilifungwa li­cha ya jitihada za uhakika kutoka kwa safu ya ulinzi inayosadikika kuwa moja ya safu bora zaidi duniani, lakini jamaa akatupia tu.

 

Mtu aliyeshuhudia kwa uka­ribu zaidi bao hilo ambaye alikuwa golini aliishia kumsifia tu. “Akiwa ka­tika ubora wake? Nadhani hakuna aliyewahi kuwa kama Ronaldo. Mes­si na yeye (Ronaldo) wanaweza kul­inganishwa na Maradona na Pele,” anasema Gianluigi Buffon, kipa wa Juve.

Hakika Ronaldo inaoneka­na alizaliwa kwa ajili ya kuja kufanya maa­jabu kwenye Ligi ya Mab­ingwa Ulaya. Hata wakati akiwa na ukame kwenye La Liga, a l i e n ­delea kuwa hatari Ulaya msimu huu wa 2017-18.

 

Kwa mwendo wake huu wa kutu­pia mabao bila kuhurumia wapinza­ni wake, Ronaldo anaelekea kuvunja rekodi yake mwenyewe ya kufunga mabao 17 katika msimu mmoja, na kuna kila dalili kwamba atatwaa tuzo yake ya sita ya Ballon d’Or (Mchezaji Bora wa Dunia) kama Real Madrid itatwaa taji la Ligi ya Mabingwa kwa mwaka wa tatu mfululizo.

 

Pia msimu huu ameweka rekodi mbili mpya: Jumanne alifanikiwa kuwa mchezaji wa kwanza kufunga bao kwenye mechi 10 mfululizo za Ligi ya Mabingwa Ulaya, na alifunga katika kila mechi kwenye hatua ya makundi, suala ambalo halikuwahi kufanyika kabla.

Ronaldo inawezekana akapata tena Tuzo ya Puskas, ambayo ni ya bao bora zaidi duniani, aliwahi kui­pata mwaka 2009 baada ya kufunga bonge la bao katika Ligi ya Mab­ingwa dhidi ya Porto.

Ronaldo anaelekea kubeba taji lake la nne la Ligi ya Mabingwa aki­wa na Real Madrid, na la tano kwake kiujumla.

 

“Unyenyekevu ukizidi siyo vizuri,” alisema Ronaldo kabla ya fainali ya msimu uliopita. “Tunatakiwa kuthibi­tisha sifa yetu na tuwaonyeshe nani ni bora zaidi. Tunaweza kupata mataji mawili, kutetea ubingwa (wa La Liga) na kuingia katika historia ya Ligi ya Mabingwa. Kuna kichocheo kikubwa na tumebakiza hatua moja.”

Kuna hatua mbili na nusu zime­baki kwa ajili ya Madrid kugeuza mataji mawili mfululizo ya Uefa kuwa matatu mfululizo, lakini ugwiji wa Ronaldo katika mi­chuano hii, umeshathibitishwa hata kama hawatatwaa taji hili.

Comments are closed.