Rasmi: De Gea Aondoka Manchester United Baada ya Miaka 12
Kipa David de Gea (32) anaondoka Manchester United baada ya kuitumikia Klabu hiyo kwa Miaka 12 ambapo Mkataba wake wa kukaa Old Trafford umemalizika mwishoni mwa Mwezi Juni 2023
Awali, iliripotiwa kuwa Mashetani Wekundu wamekubaliana Mkataba mpya na Kipa huyo, kabla ya kuachilia mbali makubaliano hayo na kuanza kufuatilia uwezekano wa kusajili Kipa wa Inter Milan, André Onana
Tangu ajiunge Man Utd akitokea Atlético Madrid mwaka 2011, De Gea amecheza Michezo 545 na kutoruhusu magoli katika Michezo 190. Ameshinda Ligi Kuu England, Kombe la FA, Ligi ya Europa na Vikombe viwili vya Carabao.